1. TASAFIC inatoa ufadhili wa masomo?
Jibu: Hapana, TASAFIC haitoi ufadhili wa masomo. Walakini, inatoa miongozo ya kusaidia wanafunzi kuelewa jinsi ya kutuma maombi ya masomo.
2. Je TASAFIC inalipa gharama za matibabu ya wanafunzi?
Jibu: Hapana. Kwa kawaida, kila mwanafunzi nchini China ana bima ya afya. Iwapo mwanafunzi atahitaji kiasi fulani cha fedha kwa ajili ya matibabu na hawezi kukipata, jumuiya yake itachukua hatua. Iwapo jamii haitaweza kusaidia suala hilo litapelekwa TASAFIC kuona iwapo mfuko wa Shirikisho unaweza kuchangia. Shirikisho likiona ugumu suala hilo litapelekwa kwa Mheshimiwa Balozi.
3. Je, una sifa gani za kuwa kiongozi katika TASAFIC?
Jibu: Kuwa kiongozi wa Jumuiya ndiyo sifa kuu ya kugombea nafasi maalum katika shirikisho. Zaidi ya hayo, lazima uwe kiongozi anayekidhi vigezo vingine, kama vile kuwa ndani ya muda wa masomo unaokuruhusu kuwahudumia wanafunzi, na kuwa na bidii na nidhamu ya hali ya juu.
4. Ninawezaje kupata taarifa za mawasiliano kwa ubalozi?
Jibu: Katika tovuti ya ubalozi, kuna mawasiliano unaweza kutumia kama vile:
Email: beijing@nje.go.tz
Phone: +86 10 6532 1408
5. Je, ninawezaje kuwasilisha ripoti au changamoto kwa ubalozi?
Jibu: Kupitia viongozi wa SHIRIKISHO, unaweza kuwasilisha changamoto, mapendekezo, au maswali. Uongozi wa Shirikisho utaweza kuwapeleka ubalozini.
6. Je, ninatakiwa kulipa ada ya TASAFIC?
Jibu: Ndiyo, ada hii haichangiwi moja kwa moja kwenye TASAFIC. Michango hii inakusanywa na jumuiya, ambayo itawasilisha michango hiyo kwa mujibu wa katiba ya shirikisho.
7. Je, ninawezaje kutoa ushauri, mapendekezo, au maoni kwa TASAFIC?
Jibu: Kupitia barua pepe, tovuti, au viongozi wa Shirikisho, unaweza kuwasilisha chochote wakati wowote.
8. Nifanye nini nikipata dharura?
Jibu: Unapaswa kwanza kuwasiliana na viongozi wa jumuiya yako. Suala hilo likihitaji umakini zaidi lifikishwe kwa viongozi wa TASAFIC. Ikihitaji hatua zaidi, itapelekwa kwa Mheshimiwa Balozi.
